Get premium membership and access revision papers with marking schemes, video lessons and live classes.
  OR
Processing. Please wait.

 Maswali na majibu ya tumbo lisiloshiba na hadithi zingine

Onyesha jinsi maudhui ya utabaka na mapenzi yanavyojitokeza katika hadithi ya “Mapenzi ya Kifaurongo”.

 (7m 7s)
15882 Views     SHARE

Download as pdf file

Answer Text:
Onyesha jinsi maudhui ya utabaka na mapenzi yanavyojitokeza katika hadithi ya “Mapenzi ya Kifaurongo”.(Al.10)
Utabaka
Katika vyuo vikuu kuna matabaka mawili la walalahai na walalahoi.
Kuna walio na chochote wanachokihitaji, mavazi laini ya vitambaa vya Hariri,
kutoka Uingereza, Ujerumani n.k na kuna wale kama Dennis Machora wanaotandika shuka kitandani zilizozeeka na kuchanikachanika. Kuna walio na simu za thamani, vipakatalishi na Ipad na wengine kama msimulizi ana kiredio kinachotoa sauti ya chini. Kuna wanaotumiwa pesa na wazazi wao mfano, Penina anayepokea elfu tano
kila wiki kukidhi mahitaji yake na kuna wale kama msimulizi ambaye hana pesa hata angalau za kununua chakula. Kuna wale ambao wazazi wao wazazi wanacho mfano Penina ni bintiye Bw Kitiwe katibu wa kudumu katika Wizara ya Fedha, lakini wazazi wake msimulizi kila asubuhi waamkapo, mipini ya majembe huwa
mabegani kazi yao kubwa ni kutafuta vibarua.
Mapenzi
Mapenzi ya kisasa yameambatanishwa na mali na kufanywa kitu kimoja pasi mapeni hakuna mapenzi. Wanafunzi wanapoenda vyuoni kila mmoja hujiingiza katika mapenzi, kama jinsi hali ilivyosawiriwa katika jumba la makazi la Mastula
Hall (uk.16) kila mtu na mpenziwe. Kuna kiu cha mapenzi kinachomfanya Penina kwenda kwa Dennis Machora na kumwomba uchumba baada ya kujua jina lake. Kuna mapenzi ya dhati vyuoni, yaani hayadumu baada ya chuo; watu wanapopatana na uhalisia wa mambo kama vile kukosa kazi. Kuna mapenzi kutoka kwa wazazi: mfano
msimulizi ana mapenzi ya dhati na wazazi waliojitaabisha kwa ajili yake.


|