Get premium membership and access revision papers with marking schemes, video lessons and live classes.
  OR
Processing. Please wait.

 Maswali na majibu ya tumbo lisiloshiba na hadithi zingine

Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika diwani ya, ‘Tumbo lisiloshiba na hadithi nyingine.’ Jadili maudhui ya nafasi ya wazazi katika malezi.

 (5m 56s)
7466 Views     SHARE

Download as pdf file

Answer Text:
Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika diwani ya, ‘Tumbo lisiloshiba na hadithi nyingine.’ Jadili maudhui ya nafasi ya wazazi katika malezi.
-Tulipokutana Tena
-Wazazi wa Bogoa - ni walezi wema ingawa ni maskini hawataki. Bogoa alelewe na wazazi wengine
Mapenzi kifaurongo:
-wazazi wa Penina Bw & Bi Kitane) wamewajibika katika kumlea Penina. Wanampa fedha za kutosha kila wiki
-licha ya kuwa maskini wazazi wa Dennis wanajizatiti sana kumpeleka chuoni hadi chuo kikuu.
Shoga yake Dada ana ndevu:
-wazazi wake Safia na Lulua wanawapenda sana wanao
-wanawapeleka wanao shuleni na kuwapa safia nafasi ya kusoma pale nyumbani
-wazazi hawa pia wana mapuuza. Wanamwamini mwanao kupita kiasi
Mame Bakari:
-babake Sara ni mkali sana, Sara anapobakwa anaogopa kumwambia kuwa ana ujauzito
-baadaye anabadilika wa kuwa mpole, anamfariji
-mamake Sara ni dhaifu, hawezi kumsaidia Sara
Ndoto ya Mashaka:
-wazazi wa Samueli wanajinyima ili kuwasomesha watoto wao
-Babake Samueli aliuza ng’ombe wengi ili kumsomesha Samueli
-mamake Samueli anatumiwa kuonyesha mapenzi ya mzazi ni ya kudumu
-babake Samueli anatumiwa kuonyesha kukata tamaa / kutamauka


|