Get premium membership and access revision papers with marking schemes, video lessons and live classes.
  OR
Processing. Please wait.

 Maswali na majibu ya tumbo lisiloshiba na hadithi zingine

a) Anwani ya hadithi TUMBO LISILOSHIBA ni mwafaka kwa hadithi hii. Fafanua (Alama 10)
b) Fafanua sifa kumi za mzee Mago (Alama 10)

 (9m 10s)
2277 Views     SHARE

Download as pdf file

Answer Text:
a) Anwani ya hadithi TUMBO LISILOSHIBA ni mwafaka kwa hadithi hii. Fafanua (Alama 10)
Tumbo lisiloshiba ni hadithi iliyopewa anwani inayosadifu yanayotendeka hadithini kwa sababu:
-Jiji licha ya kwamba lina majengo mengi bado linahitaji kupanuliwa ndio sababu ardhi ya wanamadongoporomoka inapangwa kunyakuliwa.
-Jitu linalokuja mkahawani kwa mzee Mago lina tumbo lisiloshiba, linaagiza lipewe vyakula vyote vilivyokuwa vimeandaliwa wateja wengine, pia linakunywa chupa kadhaa za soda.
-Jitu linaapa na kuahidi kuwa lingehitaji chakula maradufu zaidi siku iliyofuata. Jambo lililowashangaza kina mzee Mago na wenzake.
-Jitu lilikuja siku iliyofuata kunyakua ardhi ya
madongoporomoka. Hili linaashiria kuwa tumbo halishibi si chakula tu mbali rasilimali za raia kama ardhi.
-Tumbo lisiloshiba linasimamia wenye mamlaka ambao hawatosheki. Wanamiliki mali nyingi lakini bado wanahitaji kumiliki kidogo walicho nacho wanyonge
b) Fafanua sifa kumi za mzee Mago (Alama 10)
i) Mwenye bidii – anajitahidi kupigania haki za wanamadongoporomoka.
Ana mkahawa madongoporomoka.
ii) Mtetezi/mpenda haki – Anatafuta wakili ambaye hajahongwa ili kutetea haki ya wanyonge.
Hapuuzi uvumi kuhusu uwezekano wa vipande vyao vya ardhi kuchukuliwa.
iii) Mwenye hekima/busara – Anafahamu vyema matokeo ya
wingu linalotarajiwa kupigania haki zao.
iv) Amepevuka/mwerevu – Anafahamu uzito wa kesi unaotokana na ardhi.
v) Mzinduzi – Aliwazindua wenzake na kuwapa nasaha kuhusu maendeleo.
vi) Jasiri – Analijibu jiyu kwa kuliambia wanamadongoporomoka hawataondoka.
vii) Mshawishi – Aliwashawishi wanyonge wenzake watafute wanasheria waaminifu ili wasaidie kufafanua vipengele vigumu vya sharia.
ix) Mpenda ushirikiano – Anashirikiana na wanyonge wenzake katika kutafuta uvumbuzi wa kunyakuliwa kwa ardhi yao.
x) Mwenye matumaini – Aliamini ardhi ya wanamadongoporomoka itabaki mikononi mwao.


|