Get premium membership and access revision papers with marking schemes, video lessons and live classes.
  OR
Processing. Please wait.

 Uchambuzi wa Tumbo Lisiloshiba: Mapenzi Ya Kifaurongo (Kenna Wasike)

Bwana na Bi. Kitime na sifa zao katika hadithi Mapenzi ya Kifaurongo

 (5m 54s)
1419 Views     SHARE

Download as pdf file

Answer Text:
Bwana na Bi. Kitime katika hadithi “Mapenzi ya Kifaurongo”
-Hawa ni wazazi wa Penina.
-Bwana Kitime ni Katibu wa kudumu wa Wizara ya Fedha.
-Ni wakwasi, wako katika daraja la juu.
-Wanamtumia binti yao fedha za kutosha kila wiki.
-Wanampa binti yao malezi ya hali yajuu kwani wanajiweza.
-Wanawapatia Penina na Dennis masurufu yote wakielewa fika kuwa hawana kazi.
Sifa
-Ni washauri: walimtahadharisha Penina kuhusu kuolewa na mchochole asiye na kazi. Hata hivyo walimwachia Penina uhuru wa kujiamulia.
Ni wabaguzi-wanambagua Dennis akitaka kumuoa Penina.
-Ni walezi-wanamlea Penina na kumwelimisha hadi chuo kikuu Kivukoni.


|