Get premium membership and access revision papers with marking schemes, video lessons and live classes.
  OR
Processing. Please wait.

 Uchambuzi wa Riwaya ya Chozi La Heri (Assumpta K. Matei)

Mhusika Umulkheri na sifa zake katika riwaya ya chozi la heri

 (4m 13s)
7220 Views     SHARE

Download as pdf file

Answer Text:
Mhusika Umulkheri (Umu)
-Ni dadake Dick na Mwaliko.
Sifa.
a) Ni msomi.
Tunamwona kuwa anasomea Shule ya upili ya
mtende.
Uk 82.
b) Ni mwenye busara
Anapowakosa ndugu zake, anawatafuta kila mahali.(uk 111)
c)Ni mwenye upendo.
Anawapenda ndugu zake, na hivyo, anatia bidii kuwatafuta waliko kwenda, kwa kupiga ripoti kwenye kituo cha polisi. Uk 85,"fikra za ndugu zake zilimfanya kuzizima na hata kuishiwa na nguvu "
d)Mpenda haki.
-Alijitahidi kutafuta haki yake na ndugu zake, na kuamua kuulinda utu wake kwa hali na mali uk 85,"Nitapigana kwa jino na ukucha kuulinda utu wangu. Nitatafuta haki ilikojificha "
e) Mwenye bidii.
-Tunaona kuwa anaamka asubuhi na mapema kwenda kuitafuta haki yake. Uk 85


|