Get premium membership and access revision papers with marking schemes, video lessons and live classes.
  OR
Processing. Please wait.

 Uchambuzi wa Tumbo Lisiloshiba: Shogake dada ana ndevu (Alifa Chokocho)

Wahusika na sifa zao katika hadithi fupi ya Shogake Dada ana Ndevu

 (9m 22s)
8932 Views     SHARE

Download as pdf file

Answer Text:
Wahusika na sifa zao katika hadithi fupi ya “Shogake Dada ana Ndevu”
Safia
-Huyu ni binti wa Bw. Masudi na Bi. Hamida.
-Anasifika mno kwa tabia yake nzuri isiyokuwa na doa lolote
-Katika masomo yake alikuwa anaongoza darasa.
Sifa za Safia
-Ni mwenye tamaa: anatamani kufanya mapenzi na akatumia hila kutimiza lengo lake. Alikuwa amejivika ngozi ya kondoo nje, ndani mbwa mwitu.
-Ni mjanja: anatumia maarifa na hila za kila namna ili kupata fursa ya kufanya mapenzi.
-Ni mwenye hasira: Bi. Hamida anapomdadisi kuhusu hali yake ya kutapika, anapandisha hasira na kukimbia chumbani mwake.
-Ni mwongo: anadanganya kuwa ana malaria sugu
Anadanganya kuwa Kimwana anakuja ili wajadiliane kumbe anayekuja ni mvulana mwenye ndevu na wanafanya mapenzi.
-Ni muuaji: anatoa mimba na kukidhulumu kiumbe kisicho na hatia. Mambo hayakwenda sawa na yeye akafariki.
-Ana ubinafsi: anafikiria yeye tu bila kujua madhara ya kiumbe kilichomo ndani tumboni mwake.
Umuhimu wa Safia katika hadithi “Shogake Dada ana Ndevu”-Alifa Chokocho
Anatuonya kuwa ujanja na hila zina mwisho wake. Mara nyingi huwa na mwisho mbaya.
-Anawapofua vijana kuona uovu wa kuavya mimba.
-Anatumika kuonya vijana kuhusu udanganyifu.
-Anawasilisha ubaya wa unafiki miongoni mwa vijana.


|