Get premium membership and access revision papers with marking schemes, video lessons and live classes.
  OR
Processing. Please wait.

 Kiswahili Fasihi Simulizi Lessons and Notes

Maana ya Pembezi au pembejezi, Tondozi na mifano yake

 (3m 15s)
5131 Views     SHARE

Download as pdf file

Answer Text:
Pembezi/pembejezi
-Aina ya tondozi inayokusudiwa kusifu watu aina fulani katika jamii kutokana na matendo au mchango wao.
- k.v. watawala, walezi wazuri, mashujaa wa vita, waganga mashuhuri hata wapenzi waliopigania pendo lao.
Tondozi
-Utungo wa kutukuza watu, wanyama na vitu.
-k.v. watu mashuhuri, wapenzi, mifugo, miti mikubwa.
Mfano
Kipungu kipungu
Nani kama yeye?
Hashindiki kwa nia
Hashindiki kwa shabaha
Hulenga binguni
Hutia ghera kufikiwa peo
Peo zisofikika kwa wanokata tama
Kipungu, kipungu, hachi tufani za anga.


|