Get premium membership and access revision papers with marking schemes, video lessons and live classes.
  OR
Processing. Please wait.

 Kiswahili Fasihi Simulizi Lessons and Notes

Mbinu za Lugha/Fani /Tamathali za Usemi katika Fasihi.
-Maneno au vifungu vya maneno vinavyotumiwa kutia fasihi urembo ili kufanya ujumbe ueleweke vyema zaidi.

Aina za mbinu za lugha
1. Tashbihi -Ulinganishi kwa kutumia viunganishi kama, mithili, mfano na sawa.
2. Sitiari/ Istiara -Ulinganishi usio wa moja kwa moja. Mfano;huyu ni fisi.
3. Tashhisi/Uhaishaji -Kukipa kitu sifa ya uhai. Mfano;maji yalicheka
4. Taashira/ Ishara Kitu kuwakilisha kingine. Mfano;mwangaza-tumaini
5. Chuku/udamisi -Kutia chumvi au kufanya kitu kionekane kikubwa sana au kidogo sana. Mfano;kijana alitoa sauti kama kipaza sauti.

 (6m 36s)
33152 Views     SHARE

Download as pdf file


|